Is Mtwara underrated??
TZ nimekaa mikoa tofauti ( Dodoma, Dar, Iringa, Kigoma😂, Mtwara, Arusha) and nimetembelea mingine pia. Ila from my POV Mtwara ni underrated because
Kuna kila aina ya maisha mtu anaweza ishi. Ukipenda maisha ya kujishughulisha kilimo, ufugaji…. Mtwara kuna mashamba mazuri bei rahisi. Ukitaka kurelax uenjoy kama mstaafu unaweza pata apartment nzr by the beach kwa bei affordable( 400k pm, Dar ingekuwa 2-4m)
Business opportunity zipo. Sawa nakubali sio mji mkubwa kama Dsm Arusha, ila thts the good thing. Mtwara bado ni virgin unaweza anzisha biashara ukaikuza a few yrs later ukawa mogul kabisa ( Eg; kuna duka moja la nguo jina limenitoka, ni duka la kawaida sana kwa lvl za Dar kkoo au Sinza ila kwa Mtwara yeye ndo Don, na ninaamin anapata hela nzr kuliko maduka mengi Dsm)
Affordability. Hii haihitaji maelezo, mikoa ya pembezoni ni affordable sana .
Umeme. Personally nilikuwa nafanya kazi Tanesco gas power plant. And trust me nikikuambia kuwa Mtwara na mikoa ya kusini michache inayo kuwa supplied umeme wa gesi inauhafadhali mkubwa kwenye maswala ya kukatiwakatiwa umeme. Umeme ni changamoto only mwez wa 6 kukiwa na major overhaul ya Generators za Tanesco.
Social life. Ipo mid sana, kuna viwanja ila sio kama Dar…. Ila vibe lipo kiasi chake. Uchache wa watu unasababisha kupoe sanaaa. Kwa wengine ni jambo zr kwa wengine ni jambo baya so its up to you.
NB: Aya nimaoni yangu tu… feel free kusema kwa upande wako